Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wathesalonike 5:16-25 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Furahini daima,

17. salini kila wakati

18. na kuwa na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.

19. Msimpinge Roho Mtakatifu;

20. msidharau unabii.

21. Pimeni kila kitu: Zingatieni kilicho chema,

22. na kuepuka kila aina ya uovu.

23. Mungu mwenyewe anayetupatia amani awatakase nyinyi kabisa kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu – roho, mioyo na miili yenu – mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.

24. Yeye anayewaita nyinyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.

25. Ndugu, tuombeeni na sisi pia.

Kusoma sura kamili 1 Wathesalonike 5