Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 12:6-22 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko hekalu.

7. Kama tu mngejua maana ya maneno haya: ‘Nataka huruma wala si tambiko,’ hamngewahukumu watu wasio na hatia.

8. Maana Mwana wa Mtu ana uwezo juu ya Sabato.”

9. Yesu alitoka hapo, akaenda katika sunagogi lao.

10. Kulikuwa na mtu mmoja mwenye mkono uliopooza. Basi, watu wakamwuliza Yesu, “Je, ni halali kumponya mtu siku ya Sabato?” Walimwuliza hivyo wapate kisa cha kumshtaki.

11. Lakini Yesu akawaambia, “Tuseme mmoja wenu ana kondoo wake ambaye ametumbukia shimoni; je, hatamshika na kumtoa humo siku ya Sabato?

12. Lakini, mtu ana thamani kuliko kondoo! Basi, ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”

13. Kisha akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Akaunyosha, nao ukawa mzima kabisa kama ule mwingine.

14. Basi, Mafarisayo wakatoka nje, wakashauriana jinsi watakavyomwangamiza Yesu.

15. Lakini Yesu alipojua jambo hilo, akatoka mahali pale. Watu wengi walimfuata, akawaponya wagonjwa wote,

16. akawaamuru wasiwaambie watu habari zake,

17. ili yale aliyosema Mungu kwa njia ya nabii Isaya yatimie:

18. “Tazama mtumishi wangu niliyemteua,mpendwa wangu anipendezaye moyoni.Nitaiweka roho yangu juu yake,naye atatangaza hukumu yangu kwa mataifa yote.

19. Hatakuwa na ubishi wala kupiga kelele,wala sauti yake haitasikika barabarani.

20. Mwanzi uliopondeka hatauvunja,wala utambi ufukao moshi hatauzima,mpaka atakapoifanya hukumu ya haki itawale.

21. Kwake yeye mataifa yatakuwa na matumaini.”

22. Hapo watu wakamletea Yesu mtu mmoja kipofu na ambaye alikuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo. Yesu akamponya hata akaweza kusema na kuona.

Kusoma sura kamili Mathayo 12