Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9

Agano la Kale

Agano Jipya

Amosi 3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Enyi Waisraeli, sikilizeni neno Mwenyezi-Mungu alilosema dhidi yenu, enyi taifa zima alilolitoa nchini Misri:

2. “Kati ya mataifa yote ulimwenguni,ni nyinyi tu niliowachagua.Kwa hiyo nitawaadhibu nyinyi,kwa sababu ya uovu wenu wote.”

Jukumu la nabii

3. Je, watu wawili huanza safari pamoja,bila ya kufanya mpango pamoja kwanza?

4. Je, simba hunguruma porinikama hajapata mawindo?Je, mwanasimba hunguruma pangoni mwakekama hajakamata kitu?

5. Je, mtego bila chamboutamnasa ndege?Je, mtego hufyatukabila kuguswa na kitu?

6. Je, baragumu ya vita hulia mjinibila kutia watu hofu?Je, mji hupatwa na jangaasilolileta Mungu?

7. Hakika, Bwana Mwenyezi-Mungu hafanyi kitubila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.

8. Simba akinguruma,ni nani asiyeogopa?Bwana Mwenyezi-Mungu akinena,ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?

Kuangamizwa kwa Samaria

9. Tangazeni katika ikulu za Ashdodi,na katika ikulu za nchi ya Misri:“Kusanyikeni kwenye milimainayoizunguka nchi ya Samaria,mkajionee msukosuko mkubwana dhuluma zinazofanyika humo.”

10. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Watu hawa wameyajaza majumba yaovitu vya wizi na unyang'anyi.Hawajui kabisa kutenda yaliyo sawa!

11. Kwa hiyo, adui ataizingira nchi yao,atapaharibu mahali pao pa kujihami,na kuziteka nyara ikulu zao.”

12. Mwenyezi-Mungu, asema hivi: “Kama vile mchungaji ampokonyavyo simba kinywani miguu miwili tu au kipande cha sikio la kondoo, ndivyo watakavyonusurika watu wachache tu wa Israeli wakaao Samaria, ambao sasa wanalalia vitanda vizuri na matandiko ya hariri.”

13. Bwana Mungu wa majeshi asema hivi:“Sikilizeni, mkawaonye wazawa wa Yakobo:

14. Siku nitakapowaadhibu Waisraelikwa sababu ya makosa yao,nitayaharibu pia madhabahu ya mji wa Betheli.Nitazikata pembe za kila madhabahuna kuziangusha chini.

15. Nitaziharibu nyumba zote mjini na vijijini;nitazibomoa nyumba zilizopambwa kwa pembe,majumba makubwamakubwa hayatasalia hata moja.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”