Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 4:44-48 Biblia Habari Njema (BHN)

44. Hii ndiyo sheria ambayo Mose aliwapa Waisraeli.

45. Haya ndiyo maamuzi, masharti na maagizo ambayo Mose aliwaambia Waisraeli walipotoka Misri,

46. wakiwa ngambo ya mto Yordani, katika bonde lililo mbele ya Beth-peori, katika nchi iliyokuwa ya mfalme Sihoni wa Waamori, aliyetawala kutoka mjini Heshboni, ambaye Mose na Waisraeli walimshinda walipotoka Misri.

47. Waliitwaa nchi yake na nchi ya mfalme Ogu wa Bashani. Wafalme hao wawili wa Waamori walitawala huko mashariki ya mto Yordani.

48. Nchi hiyo ilienea toka Aroeri ukingoni mwa mto Arnoni, hadi mlima Sirioni yaani Hermoni,

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 4