Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 22:11-18 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mwenye nia safi na maneno mazuri,atakuwa rafiki wa mfalme.

12. Mwenyezi-Mungu hulinda elimu ya kweli,lakini huyavuruga maneno ya waovu.

13. Mvivu husema, “Siwezi kutoka nje;kuna simba huko, ataniua!”

14. Kinywa cha mwasherati ni shimo refu;anayechukiwa na Mwenyezi-Mungu atatumbukia humo.

15. Mtoto hupenda mambo ya kijinga moyoni,lakini fimbo ya nidhamu humwondolea hayo.

16. Anayemdhulumu maskini atamfanya afaidike mwishowe,anayewapa matajiri zawadi ataishia kuwa maskini.

17. Tega sikio usikie maneno ya wenye hekima,elekeza moyo wako uzingatie maarifa yangu.

18. Wewe utafurahi endapo utayaweka moyoni,na kuyakariri kila wakati.

Kusoma sura kamili Methali 22