Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 22:11-28 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mwenye nia safi na maneno mazuri,atakuwa rafiki wa mfalme.

12. Mwenyezi-Mungu hulinda elimu ya kweli,lakini huyavuruga maneno ya waovu.

13. Mvivu husema, “Siwezi kutoka nje;kuna simba huko, ataniua!”

14. Kinywa cha mwasherati ni shimo refu;anayechukiwa na Mwenyezi-Mungu atatumbukia humo.

15. Mtoto hupenda mambo ya kijinga moyoni,lakini fimbo ya nidhamu humwondolea hayo.

16. Anayemdhulumu maskini atamfanya afaidike mwishowe,anayewapa matajiri zawadi ataishia kuwa maskini.

17. Tega sikio usikie maneno ya wenye hekima,elekeza moyo wako uzingatie maarifa yangu.

18. Wewe utafurahi endapo utayaweka moyoni,na kuyakariri kila wakati.

19. Ninayependa kumfundisha leo ni wewe,ili tegemeo lako liwe kwa Mwenyezi-Mungu.

20. Nimekuandikia misemo thelathini,misemo ya maonyo na maarifa,

21. ili kukufundisha yaliyo sawa na kweli;na mtu akikuuliza uweze kumpa jibu sahihi.

22. Usimdhulumu maskini kwa kuwa ni maskini,wala usimnyime fukara haki yake mahakamani.

23. Maana Mwenyezi-Mungu atawatetea;atawapokonya maisha yao wale watakaowadhulumu.

24. Usifanye urafiki na mtu wa hasira,wala usiandamane na mwenye ghadhabu,

25. usije ukajifunza mwenendo wake,ukajinasa kabisa katika mtego.

26. Usiwe mmoja wao wenye kuweka ahadi,watu ambao hujiweka wadhamini wa madeni.

27. Ikiwa huna chochote cha kulipa,hata kitanda unacholalia kitachukuliwa!

28. Usiondoe alama ya mipaka ya zamaniambayo iliwekwa na wazee wako.

Kusoma sura kamili Methali 22