Agano la Kale

Agano Jipya

Walawi 13:37-53 Biblia Habari Njema (BHN)

37. Lakini iwapo kuhani ataona kuwa vile vipele vimepona na nywele nyeusi zimeota mahali hapo, basi, vidonda hivyo vimepona, basi, mtu huyo ni safi. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa safi.

38. “Kama mtu yeyote, awe mwanamume au mwanamke, ana alama nyeupe mwilini mwake,

39. kuhani atamwangalia mtu huyo. Iwapo kuhani ataona kuwa alama hizo ni nyeupe kiasi, huo ni upele wa kawaida; mtu huyo ni safi.

40. “Kama mwanamume amepata upara, yeye ni safi kwani ana upara tu.

41. Iwapo upara huo umetanda tangu nyuma mpaka mbele mtu huyo ana upara tu na yu safi.

42. Lakini kama kwenye kichwa penye upara au kwenye paji la uso penye upara kuna alama nyekundu-nyeupe, huo ni ukoma unaotokea kwenye upara wake kichwani au kwenye paji lake.

43. Kuhani atamwangalia. Iwapo kuhani ataona kuwa huo uvimbe ni mwekundu-mweupe kwenye upara au kwenye paji lake na unaonekana kama ukoma kwenye ngozi yake,

44. basi, mtu huyo ana ukoma; yeye ni najisi. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Ugonjwa wake upo kwenye kichwa chake.

45. “Mwenye ukoma yeyote atavaa nguo zilizochanika, nywele zake hatazichana, na mdomo wake wa juu ataufunika na atapaza sauti akisema, ‘Mimi ni najisi, mimi ni najisi.’

46. Ataendelea kuwa najisi kwa muda wote alio na ugonjwa huo. Yeye ni najisi; naye atakaa peke yake nje ya kambi.”

47. “Kama kuna namna ya upele wa ukoma kwenye vazi, liwe la sufu au kitani,

48. vazi hilo liwe limefumwa au limesokotwa kwa kitani au sufu au ni vazi la ngozi ya aina yoyote ile,

49. iwapo upele huo una rangi ya kijani au nyekundu katika vazi hilo, basi, vazi hilo lina upele. Kwa hiyo ni lazima kumwonesha kuhani.

50. Kuhani atauangalia upele huo na kuliweka vazi hilo kando kwa muda wa siku saba.

51. Siku ya saba atauangalia upele huo. Ikiwa upele huo umeenea katika vazi hilo, liwe ni la kufuma au kusokotwa au la ngozi au la ngozi ya aina yoyote ile, vazi hilo lina upele. Hivyo vazi hilo ni najisi.

52. Kuhani atalichoma moto vazi hilo kwani lina namna ya upele wa ukoma.

53. “Kama kuhani ataona kuwa upele haukuenea katika vazi, basi,

Kusoma sura kamili Walawi 13