Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29

Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 8 Biblia Habari Njema (BHN)

Wazawa wa Benyamini

1. Benyamini alikuwa na wana watano: Bela, mzaliwa wake wa kwanza, Ashbeli wa pili, Ahara wa tatu,

2. Noha wa nne na Rafa wa tano.

3. Bela naye alikuwa na wana: Adari, Gera, Abihudi,

4. Abishua, Naamani, Ahoa,

5. Gera, Shufamu na Huramu.

6. Hawa ndio wazawa wa Ehudi. Hawa walikuwa viongozi wa jamaa za wale waliokuwa wakiishi Geba, lakini wakachukuliwa mateka uhamishoni Manahathi;

7. Naamani, Ahiya na Gera. Gera, baba yake Uza na Ahihudi, ndiye aliyewaongoza kuchukua hatua hiyo.

8. Shaharaimu aliwapa talaka wake zake wawili, Hushimu na Baara na baadaye alipata watoto wa kiume nchini Moabu.

9. Alimwoa Hodeshi, naye akamzalia wana saba: Yoabu, Sibia, Mesha, Malkamu,

10. Yeuzi, Sakia, na Mirma. Hawa wanawe wote walikuja kuwa wakuu wa koo.

11. Shaharaimu na mkewe Hushimu alipata wana wengine wawili: Abitubu na Elpaali.

12. Wana wa Elpaali walikuwa watatu: Eberi, Mishamu na Shemedi ambaye aliijenga miji ya Ono na Lodi, pamoja na vijiji kandokando yake.

Wabenyamini walioishi Gathi na Aiyaloni

13. Beria na Shema walikuwa miongoni mwa jamaa ambazo zilikuwa zinaishi katika mji wa Aiyaloni, na kuwafukuza wenyeji wa Gathi.

14. Nao Ahio, Shashaki, Yeremothi,

15. Zebadia, Aradi, Ederi,

16. Mikaeli, Ishpa na Yoha ni wazawa wengine wa Beria.

17. Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi,

18. Ishnerai, Izlia na Yobabu walikuwa wazawa wa Epaali.

19. Yakimu, Zikri, Zabdi,

20. Elienai, Zilethai, Elieli,

21. Adaya, Beraya na Shimrathi walikuwa wazawa wa Shimei.

22. Ishpani, Eberi, Elieli,

23. Abdoni, Zikri, Hanani,

24. Hanania, Elamu, Anthothiya,

25. Ifdeya na Penueli walikuwa wazawa wa Shashaki.

26. Shamsherai, Sheharia, Athalia,

27. Yaareshia, Elia na Zikri walikuwa baadhi ya wazawa wa Yerohamu.

28. Hao ndio waliokuwa wakuu wa koo zao kulingana na vizazi vyao. Walikuwa wakuu na waliishi Yerusalemu.

Wabenyamini walioishi Gibeoni na Yerusalemu

29. Yeieli, alikuwa mwanzilishi wa mji wa Gibeoni. Mkewe alikuwa Maaka.

30. Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Abdoni. Wanawe wengine ni Zuri, Kishi, Baali, Nadabu,

31. Gedori, Ahio, Zekeri,

32. na Miklothi baba yake Shimea. Hawa pia waliishi Yerusalemu karibu na watu wengine wa ukoo wao.

Ukoo wa mfalme Shauli

33. Neri alimzaa Kishi, Kishi akamzaa Shauli. Shauli alikuwa na wana wanne: Yonathani, Malki-shua, Abinadabu na Eshbaali.

34. Yonathani alimzaa Merib-baali, na Merib-baali akamzaa Mika.

35. Mika alikuwa na wana wanne: Pithoni, Meleki, Terea na Ahazi.

36. Ahazi alimzaa Yehoada. Naye Yehoada aliwazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri. Zimri alimzaa Mosa.

37. Mosa alimzaa Binea, aliyemzaa Rafa, aliyemzaa Eleasa, naye Eleasa akamzaa Aseli.

38. Wana wa Aseli walikuwa sita: Majina yao ni Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Wote hawa walikuwa wana wa Aseli.

39. Nao wana wa Esheki, nduguye Aseli, walikuwa watatu. Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Ulamu, wa pili Yeushi na wa tatu Elifeleti.

40. Wana wa Ulamu walikuwa watu mashujaa sana wa vita, na wapiga upinde hodari. Alikuwa na wana na wajukuu wengi, jumla150. Hao wote waliotajwa hapo juu walikuwa wa ukoo wa Benyamini.