Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 15:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kujibu kwa upole hutuliza hasira,lakini neno kali huchochea hasira.

2. Ulimi wa mwenye hekima hueneza maarifa,lakini watu wapumbavu hububujika upuuzi.

3. Macho ya Mwenyezi-Mungu huona kila kitu,humchunguza mtu mwema na mtu mbaya.

4. Ulimi mpole ni chanzo cha uhai,lakini uovu wake huvunja moyo.

5. Mpumbavu hudharau mafundisho ya baba yake,lakini anayekubali maonyo ana busara.

6. Nyumbani mwa mwadilifu mna wingi wa mali,lakini mapato ya waovu huishia na balaa.

7. Mdomo wa mwenye hekima hueneza maarifa,lakini sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

8. Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini sala ya wanyofu humfurahisha Mungu.

Kusoma sura kamili Methali 15