Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 15 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kujibu kwa upole hutuliza hasira,lakini neno kali huchochea hasira.

2. Ulimi wa mwenye hekima hueneza maarifa,lakini watu wapumbavu hububujika upuuzi.

3. Macho ya Mwenyezi-Mungu huona kila kitu,humchunguza mtu mwema na mtu mbaya.

4. Ulimi mpole ni chanzo cha uhai,lakini uovu wake huvunja moyo.

5. Mpumbavu hudharau mafundisho ya baba yake,lakini anayekubali maonyo ana busara.

6. Nyumbani mwa mwadilifu mna wingi wa mali,lakini mapato ya waovu huishia na balaa.

7. Mdomo wa mwenye hekima hueneza maarifa,lakini sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

8. Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini sala ya wanyofu humfurahisha Mungu.

9. Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini Mungu huwapenda wale wafuatao mambo adili.

10. Adhabu kali ipo kwa wanaoacha mwenendo mwema;yeyote achukiaye kuonywa atakufa.

11. Ikiwa Mwenyezi-Mungu ajua yaliyo Kuzimu na Abadoni,mawazo ya binadamu yatawezaje kujificha mbele yake?

12. Mwenye madharau hapendi kuonywa,hatafuti kamwe maoni ya wenye busara.

13. Moyo wa furaha hungarisha uso,lakini uchungu huvunja moyo.

14. Mwenye busara hutafuta maarifa,lakini wapumbavu hujilisha upuuzi.

15. Kwa mnyonge kila siku ni mbaya,lakini kwa mwenye moyo mchangamfu ni sikukuu.

16. Afadhali kuwa na kidogo na kumcha Mwenyezi-Mungu,kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.

17. Afadhali mlo wa jioni wa mchicha na upendo,kuliko karamu ya nyama nono pamoja na chuki.

18. Mtu wa hasira mbaya husababisha ugomvi,lakini asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi.

19. Njia ya mvivu imesambaa miiba,njia ya mwaminifu ni wazi kama barabara kuu.

20. Mtoto mwenye hekima humfurahisha baba yake,lakini mpumbavu humdharau mama yake.

21. Upumbavu ni furaha kwa mtu asiye na akili,lakini mwenye busara huchagua njia iliyo sawa.

22. Mipango huharibika kwa kukosa shauri,lakini kwa washauri wengi, hufaulu.

23. Kutoa jibu sahihi hufurahisha;neno lifaalo kwa wakati wake ni jema mno!

24. Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai,ili aepe kuingia chini kuzimu.

25. Mwenyezi-Mungu huyabomoa makao ya wenye kiburi,lakini huilinda mipaka ya makao ya mjane.

26. Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,bali maneno mema humfurahisha.

27. Anayetamani faida ya ulanguzianaitaabisha jamaa yake,lakini achukiaye hongo ataishi.

28. Moyo wa mwadilifu hufikiri kabla ya kujibu,lakini kinywa cha mwovu hububujika uovu.

29. Mwenyezi-Mungu yuko mbali na watu waovu,lakini yu karibu na watu wema kuwasikiliza.

30. Macho ya huruma hufurahisha moyo,habari njema huuburudisha mwili.

31. Mtu ambaye husikiliza maonyo mema,anayo nafasi yake miongoni mwa wenye hekima.

32. Anayekataa kufundishwa anajidharau mwenyewe,bali anayekubali maonyo hupata busara.

33. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni shule ya hekima;kabla ya kuheshimika ni lazima kuwa mnyenyekevu.