Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 15:12-21 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Mwenye madharau hapendi kuonywa,hatafuti kamwe maoni ya wenye busara.

13. Moyo wa furaha hungarisha uso,lakini uchungu huvunja moyo.

14. Mwenye busara hutafuta maarifa,lakini wapumbavu hujilisha upuuzi.

15. Kwa mnyonge kila siku ni mbaya,lakini kwa mwenye moyo mchangamfu ni sikukuu.

16. Afadhali kuwa na kidogo na kumcha Mwenyezi-Mungu,kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.

17. Afadhali mlo wa jioni wa mchicha na upendo,kuliko karamu ya nyama nono pamoja na chuki.

18. Mtu wa hasira mbaya husababisha ugomvi,lakini asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi.

19. Njia ya mvivu imesambaa miiba,njia ya mwaminifu ni wazi kama barabara kuu.

20. Mtoto mwenye hekima humfurahisha baba yake,lakini mpumbavu humdharau mama yake.

21. Upumbavu ni furaha kwa mtu asiye na akili,lakini mwenye busara huchagua njia iliyo sawa.

Kusoma sura kamili Methali 15