Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 15:14-25 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Mwenye busara hutafuta maarifa,lakini wapumbavu hujilisha upuuzi.

15. Kwa mnyonge kila siku ni mbaya,lakini kwa mwenye moyo mchangamfu ni sikukuu.

16. Afadhali kuwa na kidogo na kumcha Mwenyezi-Mungu,kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.

17. Afadhali mlo wa jioni wa mchicha na upendo,kuliko karamu ya nyama nono pamoja na chuki.

18. Mtu wa hasira mbaya husababisha ugomvi,lakini asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi.

19. Njia ya mvivu imesambaa miiba,njia ya mwaminifu ni wazi kama barabara kuu.

20. Mtoto mwenye hekima humfurahisha baba yake,lakini mpumbavu humdharau mama yake.

21. Upumbavu ni furaha kwa mtu asiye na akili,lakini mwenye busara huchagua njia iliyo sawa.

22. Mipango huharibika kwa kukosa shauri,lakini kwa washauri wengi, hufaulu.

23. Kutoa jibu sahihi hufurahisha;neno lifaalo kwa wakati wake ni jema mno!

24. Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai,ili aepe kuingia chini kuzimu.

25. Mwenyezi-Mungu huyabomoa makao ya wenye kiburi,lakini huilinda mipaka ya makao ya mjane.

Kusoma sura kamili Methali 15