Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 6:21-29 Biblia Habari Njema (BHN)

21. yaweke daima moyoni mwako,yafunge shingoni mwako.

22. Yatakuongoza njiani mwako,yatakulinda wakati ulalapo,yatakushauri uwapo macho mchana.

23. Maana amri hiyo ni taa,na sheria hiyo ni mwanga.Maonyo hayo na nidhamu yatuweka njiani mwa uhai.

24. Yatakulinda mbali na mwanamke mbaya,yatakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.

25. Usimtamani mwanamke huyo kwa uzuri wake,wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.

26. Mtu hupoteza kipande cha mkate kwa malaya,lakini kwa mke wa mtu mwingine utapoteza uhai wako wote.

27. Je, waweza kuweka moto kifuanina nguo zako zisiungue?

28. Je, waweza kukanyaga makaa ya motona nyayo zako zisiungue?

29. Ndivyo alivyo mwanamume alalaye na mke wa mwenzake;yeyote anayemgusa mwanamke huyo hataacha kuadhibiwa.

Kusoma sura kamili Methali 6