Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 6 Biblia Habari Njema (BHN)

Maonyo manne

1. Mwanangu, kama umejitolea kumdhamini jirani yako,ikiwa umetoa ahadi yako kwa ajili ya mtu huyo,

2. umejibana kwa maneno yako mwenyewe,umejinasa kwa ahadi uliyofanya.

3. Ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzio,lakini mwanangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi:Mwendee mtu huyo mara moja umsihi akupe uhuru wako.

4. Jitahidi usiache macho yako yapate usingizi,wala kope za macho yako zisinzie.

5. Jiokoe kwa kujitoa katika mtego huo,mithili ya paa ama ndege amtorokavyo mwindaji.

6. Ewe mvivu! Hebu ukamchungulie sisimizi,fikiria namna yake ya kuishi ukapate hekima.

7. Sisimizi hana kiongozi, ofisa, wala mtawala;

8. lakini hujiwekea chakula wakati wa kiangazi,hujikusanyia akiba wakati wa mavuno.

9. Ewe mvivu, utalala hapo mpaka lini?Utaamka lini katika usingizi wako?

10. Wasema: “Acha nilale kidogo tu,acha nisinzie kidogo!Niache nikunje mikono nipumzike kidogo!”

11. Wakati huo umaskini utakuvamia kama mnyanganyi,ufukara utakufuata kama jambazi.

12. Mtu mwovu, mtu asiyefaa kitu,huzururazurura akisema maneno mapotovu.

13. Hukonyeza jicho kuwakosesha wengine,huparuza kwa nyayo,na kuashiria watu kwa vidole.

14. Akiwa amejaa ulaghai moyoni hutunga maovu,huzusha ugomvi kila mahali.

15. Kutokana na hayo maafa yatamvamia ghafla,ghafla atadhurika vibaya asiweze kupona tena.

16. Kuna vitu sita anavyochukia Mwenyezi-Mungu;naam, vitu saba ambavyo ni chukizo kwake:

17. Macho ya kiburi,ulimi mdanganyifu,mikono inayoua wasio na hatia,

18. moyo unaopanga mipango miovu,miguu iliyo mbioni kutenda maovu,

19. shahidi wa uongo abubujikaye uongo,na mtu achocheaye fitina kati ya ndugu.

Onyo dhidi ya uasherati

20. Mwanangu, shika maagizo ya baba yako,wala usisahau mafundisho ya mama yako;

21. yaweke daima moyoni mwako,yafunge shingoni mwako.

22. Yatakuongoza njiani mwako,yatakulinda wakati ulalapo,yatakushauri uwapo macho mchana.

23. Maana amri hiyo ni taa,na sheria hiyo ni mwanga.Maonyo hayo na nidhamu yatuweka njiani mwa uhai.

24. Yatakulinda mbali na mwanamke mbaya,yatakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.

25. Usimtamani mwanamke huyo kwa uzuri wake,wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.

26. Mtu hupoteza kipande cha mkate kwa malaya,lakini kwa mke wa mtu mwingine utapoteza uhai wako wote.

27. Je, waweza kuweka moto kifuanina nguo zako zisiungue?

28. Je, waweza kukanyaga makaa ya motona nyayo zako zisiungue?

29. Ndivyo alivyo mwanamume alalaye na mke wa mwenzake;yeyote anayemgusa mwanamke huyo hataacha kuadhibiwa.

30. Watu hawambezi sana mtu akiiba kwa sababu ya njaa;

31. lakini akipatikana lazima alipe mara saba;tena atatoa mali yote aliyo nayo.

32. Mwanamume anayezini na mke wa mtu hana akili kabisa;huyo hujiangamiza yeye mwenyewe.

33. Atapata majeraha na madharau;fedheha atakayopata haitamtoka.

34. Maana wivu wa mume humfanya kuwa mkali kabisa;wakati atakapolipiza kisasi hana cha kuhurumia.

35. Hatakubali fidia yoyote;wala kutulizwa na zawadi zako nyingi.