Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12

Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 11 Biblia Habari Njema (BHN)

Afanyavyo mwenye busara

1. Jishughulishe na biasharahata kama kwa kubahatisha;yawezekana baadayeukapata chochote kile.

2. Wagawie watu saba hata wanane sehemu yako,maana, hujui balaa litakalofika duniani.

3. Mawingu yakijaa maji, mvua hunyesha;mti ukiangukia kusini au kaskazini,hapo uangukiapo ndipo ulalapo.

4. Anayengoja upepo hatapanda mbegu,anayesubiri mawingu yatoweke, hatavuna kitu.

5. Usivyojua jinsi uhai unavyoingia katika mifupa ya mtoto tumboni mwa mamake, kadhalika huwezi kuelewa matendo ya Mungu, ambayo hufanya kila kitu.

6. Panda mbegu asubuhi na jioni usiache kupanda, maana, hujui zipi zitaota; za asubuhi, za jioni, au zote zitakuwa nzuri.

7. Mwanga wafaa, na kuliona jua kwapendeza macho.

8. Mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kuwa siku za giza zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.

Mawaidha kwa vijana

9. Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako, uchangamke wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na upeo wa macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.

10. Ondoa mahangaiko moyoni mwako, jikinge, usipate maumivu mwilini kwa sababu ujana na mwisho wa maisha ni bure kabisa.