Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 1:10-22 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Hezekia alimzaa Manase,Manase alimzaa Amoni,Amoni alimzaa Yosia,

11. Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake.Huo ulikuwa wakati Wayahudi walipopelekwa uhamishoni Babuloni.

12. Baada ya Wayahudi kupelekwa uhamishoni Babuloni,Yekonia alimzaa Shealtieli,Shealtieli alimzaa Zerubabeli,

13. Zerubabeli alimzaa Abiudi,Abiudi alimzaa Eliakimu,Eliakimu alimzaa Azori,

14. Azori alimzaa Zadoki,Zadoki alimzaa Akimu,Akimu alimzaa Eliudi,

15. Eliudi alimzaa Eleazari,Eleazari alimzaa Mathani,Mathani alimzaa Yakobo,

16. Yakobo alimzaa Yosefu, mumewe Maria mama yake Yesu aitwaye Kristo.

17. Basi, kulikuwa na vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi mpaka Wayahudi walipochukuliwa mateka Babuloni, na vizazi kumi na vinne tangu kuchukuliwa mateka mpaka wakati wa Kristo.

18. Basi, hivi ndivyo Yesu Kristo alivyozaliwa: Maria, mama yake, alikuwa ameposwa na Yosefu. Lakini kabla hawajakaa pamoja kama mume na mke, alionekana kuwa mjamzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.

19. Yosefu, mumewe, kwa vile alikuwa mwadilifu, hakutaka kumwaibisha hadharani; hivyo alikusudia kumwacha kwa siri.

20. Alipokuwa bado anawaza jambo hilo, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akamwambia, “Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, maana amekuwa mjamzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.

21. Atajifungua mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu, kwa kuwa yeye ndiye atakayewaokoa watu wake katika dhambi zao.”

22. Basi, haya yote yalitukia ili litimie lile neno Bwana alilosema kwa njia ya nabii:

Kusoma sura kamili Mathayo 1