Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31

Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 9 Biblia Habari Njema (BHN)

Hekima na upumbavu

1. Hekima amejenga nyumba yake,nyumba yenye nguzo saba.

2. Amechinja wanyama wa karamu,divai yake ameitayarisha,ametandika meza yake.

3. Amewatuma watumishi wake wa kike mjini,waite watu kutoka kwenye vilele vya miinuko:

4. “Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:

5. “Njoo ukale chakula,na unywe divai niliyotengeneza.

6. Achana na ujinga upate kuishi;fuata njia ya akili.”

7. Anayemkosoa mwenye dharau hupata matusi,amkaripiaye mwovu huishia kwa kuumizwa.

8. Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia;mwonye mwenye hekima naye atakupenda.

9. Mfunze mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima;mfundishe mwadilifu naye atazidi kuelimika.

10. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa hekima;na kumjua yule Mtakatifu ni kupata akili.

11. Kwa msaada wangu mimi Hekima siku zako zitaongezwa;utaongezewa miaka mingi maishani mwako.

12. Kama una hekima, itakufaa wewe mwenyewe;kama ukiidharau, mwenyewe utapata hasara.

13. Mwanamke mpumbavu ana kelele,hajui kitu wala hana haya.

14. Hukaa kitako mlangoni mwa nyumba yake,huweka kiti chake mahali pa juu mjini,

15. na kuwaita watu wapitao njiani,watu wanaokwenda kwenye shughuli zao:

16. “Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:

17. “Maji ya wizi ni matamu sana;mkate unaoliwa kwa siri ni mzuri sana.”

18. Lakini mjinga hajui kwamba humo mna wafu,wageni wa mwanamke huyo wamo chini Kuzimu.