Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 16 Biblia Habari Njema (BHN)

Jibu la Yobu

1. Hapo Yobu akajibu:

2. “Mambo kama hayo nimeyasikia mengi;nyinyi ni wafariji duni kabisa!

3. Mwisho wa maneno haya matupu ni lini?Au ni kitu gani kinachowachochea kujibu?

4. Kama nyinyi mngekuwa mimi, na mimi nyinyi,ningeweza kusema kama nyinyiningeweza kubuni maneno dhidi yenu,na kutikisa kichwa changu.

5. Ningeweza kuwatia moyo kwa maneno yangu,na maneno yangu ya faraja yangewatuliza.

6. “Lakini nikisema maumivu yangu hayatulii,na nikikaa kimya hayaondoki.

7. Kweli Mungu amenichakazaameharibu kila kitu karibu nami.

8. Amenifanya ninyauke, na huo ni ushindi dhidi yangu.Kukonda kwangu kumenikabilina kushuhudia dhidi yangu.

9. Amenirarua kwa hasira na kunichukia;amenisagia meno;na adui yangu ananikodolea macho.

10. Watu wananidhihaki na kunicheka;makundi kwa makundi hunizunguka,na kunipiga makofi mashavuni.

11. Mungu amenitia mikononi mwa wajeuri,na kunitupa mikononi mwa waovu.

12. Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;alinifanya shabaha ya mishale yake,

13. akanipiga mishale kutoka kila upande.Amenipasua figo bila huruma,na nyongo yangu akaimwaga chini.

14. Hunivunja na kunipiga tena na tena;hunishambulia kama askari.

15. “Nimejishonea mavazi ya gunia,fahari yangu nimeibwaga mavumbini.

16. Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,kope zangu zimekuwa nyeusi ti;

17. ingawa sijafanya dhuluma kwa mkono wangu,na sala zangu kwa Mungu ni safi.

18. “Ewe dunia, usiifunike damu yangu iliyomwagika;kilio changu kienee kila mahali.

19. Nina hakika ninaye shahidi wangu mbinguni,mwenye kunitetea yuko huko juu.

20. Rafiki zangu wanidharau;nabubujika machozi kumwomba Mungu.

21. Laiti mtu angenitetea mbele ya Mungu,kama ifanyikavyo duniani kati za watu wawili.

22. Naam, miaka yangu ni michache,nami nitakwenda huko ambako sitarudi.