Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 19 Biblia Habari Njema (BHN)

Jibu la Yobu

1. Kisha Yobu akajibu:

2. “Mtaendelea kunitesa mpaka lini,na kunivunjavunja kwa maneno?

3. Mara hizi zote kumi mmenishutumu.Je, hamwoni aibu kunitendea vibaya?

4. Hata kama ingekuwa nimekosa kweli,kosa langu lanihusu mimi mwenyewe.

5. Mnaishusha hadhi yangu mpate kujikuza;mnanilaumu kwa kunyenyekezwa kwangu.

6. Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,na kuninasa katika wavu wake.

7. Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’Lakini sijibiwi.Naita kwa sauti kubwa,lakini sipati haki yangu.

8. Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipiteamezitia giza njia zangu.

9. Amenivua fahari yangu;ameiondoa taji yangu kichwani.

10. Amenivunja pande zote, nami nimekwisha;tumaini langu amelingoa kama mti.

11. Ameichochea ghadhabu yake dhidi yangu;ameniona kuwa kama adui yake.

12. Majeshi yake yanijia kwa pamoja;yametengeneza njia ya kuja kwangu,yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.

13. Mungu amewaweka ndugu zangu mbali nami;rafiki zangu wakuu wamenitoroka kabisa.

14. Jamaa zangu na marafiki hawanisaidii tena.

15. Wageni nyumbani mwangu wamenisahau;watumishi wangu wa kike waniona kuwa mgeni.Mimi nimekuwa kwao mtu wasiyemjua.

16. Namwita mtumishi wangu lakini haitikii,ninalazimika kumsihi sana kwa maneno.

17. Nimekuwa kinyaa kwa mke wangu;chukizo kwa ndugu zangu mwenyewe.

18. Hata watoto wadogo hunidharau,mara ninapojitokeza wao hunizomea.

19. “Rafiki zangu wakuu wanachukizwa nami,wale niliokuwa nikiwapenda wamenipa kisogo.

20. Mwili wangu umebakia tu mifupa na ngozi,nimeponea chupuchupu baada ya kupoteza yote.

21. Nioneeni huruma,nioneeni huruma enyi rafiki zangu;maana mkono wa Mungu umenifinya.

22. Kwa nini mnanifuatia kama Mungu?Mbona hamtosheki na mwili wangu?

23. “Laiti maneno yangu yangeandikwa!Laiti yangeandikwa kitabuni!

24. Laiti yangechorwa kwa chuma na risasijuu ya jiwe ili yadumu!

25. Najua wazi Mkombozi wangu anaishi,mwishowe yeye atanipa haki yangu hapahapa duniani.

26. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivyo,nitamwona Mungu kwa macho yangu mwenyewe.

27. Mimi mwenyewe nitakutana naye;mimi mwenyewe na si mwingine nitamwona kwa macho.

28. “Nyinyi mwaweza kujisemea:‘Tutamfuatia namna gani?

29. Tutapataje kwake kisa cha kumshtaki?’Lakini tahadharini na adhabu.Chuki yenu yaweza kuwaletea kifo!Mnapaswa kujua: Mungu peke yake ndiye hakimu.”