Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 20 Biblia Habari Njema (BHN)

Hoja ya tatu ya Sofari

1. Kisha Sofari, Mnaamathi, akajibu:

2. “Fikira zangu zanifanya nikujibu,wala siwezi kujizuia tena.

3. Nasikia maonyo nisiyoweza kuvumilia,lakini akili yangu yanisukuma nijibu.

4. “Wewe labda umesahau jambo hili:Kwamba tangu zamani Mungu alipomuumba mtu duniani,

5. mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu,furaha yake asiyemcha Mungu ni ya muda mfupi tu!

6. Mwovu aweza kufana hata kufikia mbingu,kichwa chake kikafika kwenye mawingu,

7. lakini atatupiliwa mbali kama mavi yake.Waliopata kumjua watajiuliza: ‘Yuko wapi?’

8. Atatoweka kama ndoto, asionekane tena,atafutika kama maono ya usiku.

9. Aliyemwona, hatamwona tena,wala pale alipoishi hapatatambuliwa tena.

10. Yeye mwenyewe itambidi kurudisha mali yake yote,watoto wake wataomba huruma kwa maskini.

11. Japo alijisikia amejaa nguvu za ujana,lakini zote zitalala pamoja naye mavumbini.

12. “Mdomoni mwake uovu ni mtamu kama sukari,anauficha chini ya ulimi wake;

13. hataki kabisa kuuachilia,bali anaushikilia kinywani mwake.

14. Lakini ufikapo tumboni huwa mchungu,mkali kama sumu ya nyoka.

15. Mwovu humeza mali haramu na kuitapika;Mungu huitoa tumboni mwake.

16. Anachonyonya mtu mwovu ni sumu ya nyoka;atauawa kwa kuumwa na nyoka.

17. Hataishi kuiona mitiririko ya fanaka,wala vijito vya mafanikio na utajiri.

18. Matunda ya jasho lake atayaachilia,hatakuwa na uwezo wa kuyaonja,

19. kwa sababu amewaangamiza maskini na kuwaacha,amenyakua nyumba ambazo hakuzijenga.

20. “Kwa vile ulafi wake hauna mwisho,hataweza kuokoa chochote anachothamini.

21. Baada ya kula hakuacha hata makombo,kwa hiyo fanaka yake yote haitadumu.

22. Kileleni mwa fanaka dhiki itamvamia,balaa itamkumba kwa nguvu zote.

23. Akiwa anajishughulisha kushibisha tumbo,Mungu atamletea ghadhabu yakeimtiririkie kama chakula chake.

24. Labda ataweza kuepa upanga wa chuma,kumbe atachomwa na upanga wa shaba.

25. Mshale utachomolewa kutoka mwilini mwake;ncha yake itatolewa mgongoni mwake ikingaa,vitisho vya kifo vitamvamia.

26. Hazina zake zitaharibiwa,moto wa ajabu utamteketeza;kilichobaki nyumbani mwake kitateketezwa.

27. Mbingu zitaufichua uovu wake,dunia itajitokeza kumshutumu.

28. Mali zake zitanyakuliwakatika siku ya ghadhabu ya Mungu.

29. Hicho ndicho apewacho mtu mwovu kutoka kwa Mungu,ndicho mwovu alichopangiwa na Mungu.”