Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42

Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 39 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Je, wajua mbuzi wa milimani huzaa lini,au umewahi kuona kulungu akizaa?

2. Je, wajua huchukua mimba kwa muda gani,au siku yenyewe ya kuzaa waijua?

3. “Wajua wakati watakapochuchumaa kuzaa,wakati wa kuzaa watoto wao?

4. Watoto wao hupata nguvu,hukua hukohuko porini,kisha huwaacha mama zao na kwenda zao.

5. “Nani aliyemwacha huru pundamwitu?Nani aliyewaacha waende kwa kuwafungua?

6. Mimi niliwapa jangwa liwe makao yao,mbuga zenye chumvi kuwa makazi yao.

7. Hujitenga kabisa na makelele ya miji,hasikilizi kelele ya kumfanyisha kazi.

8. Hutembeatembea milimani kupata malisho,na kutafuta chochote kilicho kibichi.

9. “Je, nyati atakubali kukutumikia?Au je, atakubali kulala zizini mwako?

10. Je, waweza kumfunga nyati kamba kulima shamba,au avute jembe la kulimia?

11. Je, utamtegemea kwa kuwa ana nguvu nyingina kumwacha akufanyie kazi zako nzito?

12. Je, wamtazamia nyati akuvunie mavuno yako,na kuleta nafaka mahali pa kupuria?

13. “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa madaha,lakini hawezi kuruka kama korongo.

14. Mbuni huyaacha mayai yake juu ya ardhiili yapate joto mchangani;

15. lakini hajui kama yanaweza kukanyagwa,au kuvunjwa na mnyama wa porini.

16. Mbuni huwatendea wanawe ukatili kama si wake,hata kazi yake ikiharibika yeye hana wasiwasi;

17. kwa sababu nilimfanya asahau hekima yake,wala sikumpa sehemu yoyote ya akili.

18. Lakini akianza kukimbia,humcheka hata farasi na mpandafarasi.

19. “Je, Yobu, ndiwe uliyewapa farasi nguvu,ukawavika shingoni manyoya marefu?

20. Je, ni wewe unayemfanya farasi aruke kama nzige?Mlio wake wa maringo ni wa ajabu!

21. Huparapara ardhi mabondeni kwa pupa;hukimbilia kwenye mapigano kwa nguvu zake zote.

22. Farasi huicheka hofu, na hatishiki;wala upanga hauwezi kumrudisha nyuma.

23. Silaha wachukuazo wapandafarasi,hugongana kwa sauti na kungaa juani.

24. Farasi husonga mbele, akitetemeka kwa hasira;tarumbeta iliapo, yeye hasimami.

25. Kila ipigwapo tarumbeta, yeye hutoa sauti;huisikia harufu ya vita toka mbali,huusikia mshindo wa makamandawakitoa amri kwa makelele.

26. “Je, mwewe amejifunza kwako jinsi ya kuruka,na kunyosha mabawa yake kuelekea kusini?

27. Je, tai hupaa juu kwa amri yako,na kuweka kiota chake juu milimani?

28. Tai hufanya makazi yake juu ya miamba mirefu,na ncha kali za majabali ndizo ngome zake.

29. Kutoka huko huotea mawindo,macho yake huyaona kutoka mbali.

30. Makinda yake hufyonza damu;pale ulipo mzoga ndipo alipo tai.”