Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 2 Biblia Habari Njema (BHN)

Amani ya kudumu

1. Neno alilopewa Isaya, mwana wa Amozi, kuhusu Yuda na Yerusalemu.

2. Siku zijazo mlima wa nyumba ya Mwenyezi-Munguutaimarishwa kupita milima yote,utainuliwa juu ya vilima vyote.Mataifa yote yatamiminika huko,

3. watu wengi wataujia na kusema,“Njoni tupande mlima wa Mwenyezi-Mungu,twende nyumbani kwa Mungu wa Yakobo,apate kutufundisha njia zake,nasi tuishi kadiri ya mwongozo wake.Maana sheria itakuja kutoka Siyoni;neno la Mwenyezi-Mungu kutoka Yerusalemu.”

4. Mungu atasuluhisha mizozo ya mataifaatakata mashauri ya watu wengi.Watu watafua panga za vita kuwa majembena mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea.Taifa halitapigana na taifa linginewala hayatafanya tena mazoezi ya vita.

5. Sasa, enyi wazawa wa Yakobo, njoni,tutembee katika mwanga wa Mwenyezi-Mungu.

Kiburi kitaondolewa

6. Sasa, ee Mungu, umewatupa watu wako, wazawa wa Yakobo.Maana kweli wachawi wa mashariki wamejaa kati yao,wapo na wapiga ramli kama kwa Wafilisti.Wanashirikiana na watu wageni.

7. Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,hazina yao ni kubwa kupindukia.Nchi yao imejaa farasi,magari yao ya kukokotwa hayana idadi.

8. Nchi yao imejaa vinyago vya miungu,huabudu kazi ya mikono yao,vitu walivyotengeneza wao wenyewe.

9. Kwa hiyo, kila mtu ataaibishwa na kufedheheshwa.Usiwasamehe hata kidogo, ee Mungu!

10. Ingieni katika mwamba,mkajifiche mavumbini,kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,mbali na utukufu wa enzi yake.

11. Siku yaja ambapo kiburi cha watu kitashushwa,majivuno ya kila mtu yatavunjwa;na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.

12. Naam, yaja siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshidhidi ya wenye kiburi na majivuno,dhidi ya wote wanaojikweza;

13. dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni,ambayo ni mirefu na mizuri,dhidi ya mialoni yote nchini Bashani;

14. dhidi ya milima yote mirefu,dhidi ya vilima vyote vya juu;

15. dhidi ya minara yote mirefu,dhidi ya kuta zote za ngome;

16. dhidi ya meli zote za Tarshishi,na dhidi ya meli zote nzuri.

17. Kiburi chote cha watu kitakomeshwa,majivuno ya kila mtu yatavunjwa.Na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.

18. Vinyago vyote vya miungu vitatoweka kabisa.

19. Ingieni katika mapango miambani,katika mashimo ardhini,kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,mbali na utukufu wa enzi yake,atakapokuja kuitia hofu dunia.

20. Siku hiyo, watu watawatupia panya na popovinyago vyao vya fedha na dhahabuwalivyojitengenezea ili kuviabudu.

21. Nao wataingia katika mapango miambanina kwenye nyufa za miamba,kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,mbali na utukufu wa enzi yake,atakapokuja kuitia hofu dunia.

22. Usimwamini binadamu,uhai wake haudumu kama pumzi.Yeye anafaa kitu gani?