Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 35 Biblia Habari Njema (BHN)

Furaha ijayo ya Yerusalemu

1. Nyika na nchi kavu vitachangamka,jangwa litafurahi na kuchanua maua.

2. Litachanua maua kwa wingi kama waridi,litashangilia na kuimba kwa furaha.Mungu atalijalia fahari ya milima ya Lebanoni,uzuri wa mlima Karmeli na wa bonde la Sharoni.Watu watauona utukufu wa Mwenyezi-Mungu,watauona ukuu wa Mungu wetu.

3. Imarisheni mikono yenu dhaifu,kazeni magoti yenu manyonge.

4. Waambieni waliokufa moyo:“Jipeni moyo, msiogope!Tazameni Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi,atakuja kuwaadhibu maadui zenu;atakuja yeye mwenyewe kuwaokoeni.”

5. Hapo vipofu wataona tena,na viziwi watasikia tena.

6. Walemavu watarukaruka kama paa,na bubu wataimba kwa furaha.Maji yatabubujika nyikanina vijito vya maji jangwani.

7. Mchanga wa moto jangwani utakuwa bwawa la maji,ardhi kavu itabubujika vijito vya maji.Makao ya mbwamwitu yatajaa maji;nyasi zitamea na kukua kama mianzi.

8. Humo kutakuwa na barabara kuu,nayo itaitwa “Njia Takatifu.”Watu najisi hawatapitia humo,ila tu watu wake Mungu;wapumbavu hawatadiriki kuikanyaga,

9. humo hakutakuwa na simba,mnyama yeyote mkali hatapitia humo,hao hawatapatikana humo.Lakini waliokombolewa ndio watakaopita humo.

10. Waliokombolewa na Mwenyezi-Mungu watarudi,watakuja Siyoni wakipiga vigelegele.Watakuwa wenye furaha ya milele,watajaliwa furaha na shangwe;huzuni na kilio vitatoweka kabisa.