Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66

Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 14 Biblia Habari Njema (BHN)

Kurudi kutoka uhamishoni

1. Mwenyezi-Mungu atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawateua tena Waisraeli. Atawarudisha katika nchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.

2. Watu wa mataifa watawasaidia Waisraeli kurudi katika nchi waliyopewa na Mwenyezi-Mungu. Na hapo watawatumikia Waisraeli kama watumwa. Wale waliowateka sasa watatekwa na Waisraeli, na watawatawala wale waliowadhulumu.

Mfalme wa Babuloni miongoni mwa wafu

3. Ewe Israeli, wakati Mwenyezi-Mungu atakapokufariji baada ya mateso, misukosuko na utumwa uliofanyiwa,

4. utaimba utenzi huu wa kumdhihaki mfalme wa Babuloni:“Jinsi gani mdhalimu alivyokomeshwa!Ujeuri wake umekomeshwa!

5. Mwenyezi-Mungu amelivunja gongo la waovu,ameivunja fimbo ya kifalme ya watawala,

6. ambao walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma,na kuwatawala kwa udhalimu bila huruma.

7. Sasa dunia yote ina utulivu na amani,kila mtu anaimba kwa furaha.

8. Misonobari inafurahia kuanguka kwako,nayo mierezi ya Lebanoni pamoja yasema:‘Kwa vile sasa umeangushwa,hakuna mkata miti atakayekuja dhidi yetu!’

9. “Kuzimu nako kumechangamka,ili kukulaki wakati utakapokuja.Kunaiamsha mizimu ije kukusalimuna wote waliokuwa wakuu wa dunia;huwaamsha kutoka viti vyao vya enziwote waliokuwa wafalme wa mataifa.

10. Wote kwa pamoja watakuambia:‘Nawe pia umedhoofika kama sisi!Umekuwa kama sisi wenyewe!

11. Fahari yako imeteremshwa kuzimupamoja na muziki wa vinubi vyako.Chini mabuu ndio kitanda chako,na wadudu ndio blanketi lako!’

12. “Jinsi gani ulivyoporomoshwa toka mbinguni,wewe uliyekuwa nyota angavu ya alfajiri.Jinsi gani ulivyoangushwa chini,wewe uliyeyashinda mataifa!

13. Wewe ulijisemea moyoni mwako:‘Nitapanda mpaka mbinguni;nitaweka kiti changu juu ya nyota za Mungu,nitaketi juu ya mlima wakutanapo miungu,huko mbali pande za kaskazini.

14. Nitapanda vilele vya mawingunitajifanya kuwa sawa na Mungu Mkuu.’

15. Lakini umeporomoshwa hadi kuzimu;umeshushwa chini kabisa shimoni.

16. “Watakaokuona watakukodolea macho,watakushangaa wakisema:‘Je, huyu ndiye aliyetetemesha duniana kuzitikisa falme,

17. aliyegeuza dunia kuwa kama jangwa,akaangamiza miji yake,na kuwanyima wafungwa wake kurudi kwao?’

18. Wafalme wote wa mataifa wamezikwa kwa heshimakila mmoja ndani ya kaburi lake.

19. Lakini wewe umetupwa nje ya kaburi lako;kama mtoto wa kuchukiza aliyezaliwa mfumaiti yako imekanyagwakanyagwa,umerundikiwa maiti za waliouawa kwa upanga,waliotupwa mashimoni penye mawe.

20. Lakini wewe hutaunganishwa nao katika mazishi,maana uliiharibu nchi yako,wewe uliwaua watu wako.Wazawa wa waovu na wasahaulike kabisa!

21. Kaeni tayari kuwachinja watoto wakekwa sababu ya makosa ya baba zao,wasije wakaamka na kuimiliki nchi,na kuijaza dunia yote miji yao.”

Mungu ataangamiza Babuloni

22. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Nitaushambulia mji wa Babuloni na kuuangamiza kabisa. Nitaharibu kila kitu, mji wote, watoto na yeyote aliyebaki hai. Mimi Mwenyezi-Mungu nimenena.

23. Nitaufanya kuwa makao ya nungunungu, na utakuwa madimbwi ya maji. Nami nitaufagilia mbali kwa ufagio wa maangamizi. Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimenena.”

Mwisho wa udhalimu wote

24. Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameapa:“Kama nilivyopanga,ndivyo itakavyokuwa;kama nilivyokusudia,ndivyo itakavyokamilika.

25. Nitauvunja uwezo wa Waashuru nchini mwangu;nitawakanyagakanyaga katika milima yangu.Nitawaondolea watu wangu nira ya dhuluma yao,na mzigo wa mateso yao.”

26. Huu ndio uamuzi wake Mwenyezi-Mungukuhusu dunia yote;hii ndiyo adhabu atakayotoajuu ya mataifa yote.

27. Kama Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameamua,nani atakayeweza kubatilisha uamuzi wake?Kama amepania kutoa adhabu,ni nani atakayempinga?

Mungu atawaangamiza Wafilisti

28. Mwaka alipofariki mfalme Ahazi, Mungu alitoa kauli hii:

29. “Msishangilie enyi Wafilisti wote,kwamba Ashuru, fimbo iliyowapiga, imevunjika;maana, nyoka wa kawaida atazaa nyoka mwenye sumu,na nyoka mwenye sumu atazaa joka lirukalo.

30. Wazaliwa wa kwanza wa maskini watashiba,na fukara watakaa kwa usalama.Lakini chipukizi wenu nitawaua kwa njaa;na yeyote wenu atakayebaki nitamuua.

31. Piga yowe ewe lango; lia ewe mji;yeyuka kwa hofu ewe nchi yote ya Filistia.Maana moshi wa askari waja kutoka kaskazini,wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake.”

32. Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo?Wataambiwa: Mwenyezi-Mungu ameijenga imara Siyoni,na maskini wa watu wake watakimbilia usalama huko.