Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66
  67. 67
  68. 68
  69. 69
  70. 70
  71. 71
  72. 72
  73. 73
  74. 74
  75. 75
  76. 76
  77. 77
  78. 78
  79. 79
  80. 80
  81. 81
  82. 82
  83. 83
  84. 84
  85. 85
  86. 86
  87. 87
  88. 88
  89. 89
  90. 90
  91. 91
  92. 92
  93. 93
  94. 94
  95. 95
  96. 96
  97. 97
  98. 98
  99. 99
  100. 100
  101. 101
  102. 102
  103. 103
  104. 104
  105. 105
  106. 106
  107. 107
  108. 108
  109. 109
  110. 110
  111. 111
  112. 112
  113. 113
  114. 114
  115. 115
  116. 116
  117. 117
  118. 118
  119. 119
  120. 120
  121. 121
  122. 122
  123. 123
  124. 124
  125. 125
  126. 126
  127. 127
  128. 128
  129. 129
  130. 130
  131. 131
  132. 132
  133. 133
  134. 134
  135. 135
  136. 136
  137. 137
  138. 138
  139. 139
  140. 140
  141. 141
  142. 142
  143. 143
  144. 144
  145. 145
  146. 146
  147. 147
  148. 148
  149. 149
  150. 150

Agano la Kale

Agano Jipya

Zab. 10 Swahili Union Version (SUV)

Sala ya Ukombozi kutoka kwa Adui

1. Ee BWANA, kwa nini wasimama mbali?Kwani kujificha nyakati za shida?

2. Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali;Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza.

3. Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake,Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.

4. Mdhalimu kwa kiburi cha uso wakeAsema, Hatapatiliza.Jumla ya mawazo yake ni, Hakuna Mungu;

5. Njia zake ni thabiti kila wakati.Hukumu zako ziko juu asizione,Adui zake wote awafyonya.

6. Asema moyoni mwake, Sitaondoshwa,Kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni.

7. Kinywa chake kimejaa laana,Na hila na dhuluma.Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,

8. Hukaa katika maoteo ya vijiji.Mahali pa siri humwua asiye na hatia,Macho yake humvizia mtu duni.

9. Huotea faraghani kama simba pangoni,Huotea amkamate mtu mnyonge.Naam, humkamata mtu mnyonge,Akimkokota wavuni mwake.

10. Hujikunyata na kuinama;Watu duni huanguka kwa nguvu zake.

11. Asema moyoni mwake, Mungu amesahau,Auficha uso wake, haoni kamwe.

12. BWANA, uondoke, Ee Mungu, uuinue mkono wako,Usiwasahau wanyonge.

13. Kwani mdhalimu kumdharau Mungu.Akisema moyoni mwake, Hutapatiliza?

14. Umeona, maana unaangalia madhara na jeuri,Uyatwae mkononi mwako.Mtu duni hukuachia nafsi yake,Maana umekuwa msaidizi wa yatima.

15. Uuvunje mkono wake mdhalimu,Na mbaya, uipatilize dhuluma yake, hata usiione.

16. BWANA ndiye Mfalme milele na milele;Mataifa wamepotea kutoka nchi yake.

17. BWANA, umeisikia tamaa ya wanyonge,Utaitengeneza mioyo yao, utalitega sikio lako.