Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66
  67. 67
  68. 68
  69. 69
  70. 70
  71. 71
  72. 72
  73. 73
  74. 74
  75. 75
  76. 76
  77. 77
  78. 78
  79. 79
  80. 80
  81. 81
  82. 82
  83. 83
  84. 84
  85. 85
  86. 86
  87. 87
  88. 88
  89. 89
  90. 90
  91. 91
  92. 92
  93. 93
  94. 94
  95. 95
  96. 96
  97. 97
  98. 98
  99. 99
  100. 100
  101. 101
  102. 102
  103. 103
  104. 104
  105. 105
  106. 106
  107. 107
  108. 108
  109. 109
  110. 110
  111. 111
  112. 112
  113. 113
  114. 114
  115. 115
  116. 116
  117. 117
  118. 118
  119. 119
  120. 120
  121. 121
  122. 122
  123. 123
  124. 124
  125. 125
  126. 126
  127. 127
  128. 128
  129. 129
  130. 130
  131. 131
  132. 132
  133. 133
  134. 134
  135. 135
  136. 136
  137. 137
  138. 138
  139. 139
  140. 140
  141. 141
  142. 142
  143. 143
  144. 144
  145. 145
  146. 146
  147. 147
  148. 148
  149. 149
  150. 150

Agano la Kale

Agano Jipya

Zab. 74 Swahili Union Version (SUV)

Ombi la Kutaka Msaada Wakati wa Kushindwa

1. Ee Mungu, mbona umetutupa milele?Kwa nini hasira yako inatoka moshiJuu ya kondoo wa malisho yako?

2. Ulikumbuke kusanyiko lako,Ulilolinunua zamani.Ulilolikomboa liwe kabila ya urithi wako,Mlima Sayuni ulioufanya maskani yako.

3. Upainulie miguu yako palipoharibika milele;Adui ameufanya kila ubaya katika patakatifu.

4. Watesi wako wamenguruma kati ya kusanyiko lako;Wameweka bendera zao ziwe alama.

5. Wanaonekana kama watu wainuao mashoka,Waikate miti ya msituni.

6. Na sasa nakishi yake yote piaWanaivunja-vunja kwa mashoka na nyundo.

7. Wamepatia moto patakatifu pako;Wamelinajisi kao la jina lako hata chini.

8. Walisema mioyoni mwao,Na tuwaangamize kabisa;Mahali penye mikutano ya MunguWamepachoma moto katika nchi pia.

9. Hatuzioni ishara zetu, wala sasa hakuna nabii,Wala kwetu hakuna ajuaye, hata lini?

10. Ee Mungu, mtesi atalaumu hata lini?Adui alidharau jina lako hata milele?

11. Mbona unaurudisha mkono wako,Naam, mkono wako wa kuume,Uutoe kifuani mwako,Ukawaangamize kabisa.

12. Lakini Mungu ni mfalme wangu tokea zamani,Afanyaye mambo ya wokovu katikati ya nchi.

13. Wewe umeipasua bahari kwa nguvu zako,Umevivunja vichwa vya nyangumi juu ya maji.

14. Wewe uliviseta vichwa vya lewiathani,Awe chakula cha watu wa jangwani.

15. Wewe ulitokeza chemchemi na kijito;Wewe ulikausha mito yenye maji sikuzote.

16. Mchana ni wako, usiku nao ni wako,Ndiwe uliyeufanya mwanga na jua.

17. Wewe uliiweka mipaka yote ya dunia,Kaskazi na kusi Wewe ulizitengeneza.

18. Ee BWANA, uyakumbuke hayo, adui amelaumu,Na watu wapumbavu wamelidharau jina lako.

19. Usimpe mnyama mkali nafsi ya hua wako;Usiusahau milele uhai wa watu wako walioonewa.

20. Ulitafakari agano;Maana mahali penye giza katika nchiPamejaa makao ya ukatili.

21. Aliyeonewa asirejee ametiwa haya,Mnyonge na mhitaji na walisifu jina lako.

22. Ee Mungu, usimame, ujitetee mwenyewe,Ukumbuke unavyotukanwa na mpumbavu mchana kutwa.