Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66
  67. 67
  68. 68
  69. 69
  70. 70
  71. 71
  72. 72
  73. 73
  74. 74
  75. 75
  76. 76
  77. 77
  78. 78
  79. 79
  80. 80
  81. 81
  82. 82
  83. 83
  84. 84
  85. 85
  86. 86
  87. 87
  88. 88
  89. 89
  90. 90
  91. 91
  92. 92
  93. 93
  94. 94
  95. 95
  96. 96
  97. 97
  98. 98
  99. 99
  100. 100
  101. 101
  102. 102
  103. 103
  104. 104
  105. 105
  106. 106
  107. 107
  108. 108
  109. 109
  110. 110
  111. 111
  112. 112
  113. 113
  114. 114
  115. 115
  116. 116
  117. 117
  118. 118
  119. 119
  120. 120
  121. 121
  122. 122
  123. 123
  124. 124
  125. 125
  126. 126
  127. 127
  128. 128
  129. 129
  130. 130
  131. 131
  132. 132
  133. 133
  134. 134
  135. 135
  136. 136
  137. 137
  138. 138
  139. 139
  140. 140
  141. 141
  142. 142
  143. 143
  144. 144
  145. 145
  146. 146
  147. 147
  148. 148
  149. 149
  150. 150

Agano la Kale

Agano Jipya

Zab. 77 Swahili Union Version (SUV)

Matendo Makuu ya Mungu Yasimuliwa

1. Nimpazie Mungu sauti yangu,Naam, nimpazie Mungu, naye atanisikia.

2. Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana;Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea;Nafsi yangu ilikataa kufarijika.

3. Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika;Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia.

4. Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike;Naliona mashaka nisiweze kunena.

5. Nalifikiri habari za siku za kale,Miaka ya zamani zilizopita.

6. Nakumbuka wimbo wangu usiku,Nawaza moyoni mwangu,Roho yangu ikatafuta.

7. Je! Bwana atatupa milele na milele?Hatatenda fadhili tena kabisa?

8. Rehema zake zimekoma hata milele?Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?

9. Mungu amesahau fadhili zake?Amezuia kwa hasira rehema zake?

10. Nikasema, Ndio udhaifu wangu huo;Lakini nitaikumbuka miaka ya mkono wa kuume wake Aliye juu.

11. Nitayakumbuka matendo ya BWANA;Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale.

12. Pia nitaitafakari kazi yako yote;Nitaziwaza habari za matendo yako.

13. Ee Mungu, njia yako i katika utakatifu;Ni nani aliye mungu mkuu kama Mungu?

14. Wewe ndiwe Mungu ufanyaye maajabu;Uliudhihirisha uweza wako kati ya mataifa.

15. Kwa mkono wako umewakomboa watu wako,Wana wa Yakobo na Yusufu.

16. Ee Mungu, yale maji yalikuona,Yale maji yalikuona, yakaogopa.Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,

17. Mawingu yakamwaga maji.Mbingu nazo zikatoa sauti,Mishale yako nayo ikatapakaa.

18. Sauti ya radi yako ikawa katika kisulisuli;Umeme uliuangaza ulimwengu.Nchi ilitetemeka na kutikisika;

19. Njia yako ilikuwa katika bahari.Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu;Hatua zako hazikujulikana.