Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14
  15. 15
  16. 16
  17. 17
  18. 18
  19. 19
  20. 20
  21. 21
  22. 22
  23. 23
  24. 24
  25. 25
  26. 26
  27. 27
  28. 28
  29. 29
  30. 30
  31. 31
  32. 32
  33. 33
  34. 34
  35. 35
  36. 36
  37. 37
  38. 38
  39. 39
  40. 40
  41. 41
  42. 42
  43. 43
  44. 44
  45. 45
  46. 46
  47. 47
  48. 48
  49. 49
  50. 50
  51. 51
  52. 52
  53. 53
  54. 54
  55. 55
  56. 56
  57. 57
  58. 58
  59. 59
  60. 60
  61. 61
  62. 62
  63. 63
  64. 64
  65. 65
  66. 66
  67. 67
  68. 68
  69. 69
  70. 70
  71. 71
  72. 72
  73. 73
  74. 74
  75. 75
  76. 76
  77. 77
  78. 78
  79. 79
  80. 80
  81. 81
  82. 82
  83. 83
  84. 84
  85. 85
  86. 86
  87. 87
  88. 88
  89. 89
  90. 90
  91. 91
  92. 92
  93. 93
  94. 94
  95. 95
  96. 96
  97. 97
  98. 98
  99. 99
  100. 100
  101. 101
  102. 102
  103. 103
  104. 104
  105. 105
  106. 106
  107. 107
  108. 108
  109. 109
  110. 110
  111. 111
  112. 112
  113. 113
  114. 114
  115. 115
  116. 116
  117. 117
  118. 118
  119. 119
  120. 120
  121. 121
  122. 122
  123. 123
  124. 124
  125. 125
  126. 126
  127. 127
  128. 128
  129. 129
  130. 130
  131. 131
  132. 132
  133. 133
  134. 134
  135. 135
  136. 136
  137. 137
  138. 138
  139. 139
  140. 140
  141. 141
  142. 142
  143. 143
  144. 144
  145. 145
  146. 146
  147. 147
  148. 148
  149. 149
  150. 150

Agano la Kale

Agano Jipya

Zab. 41 Swahili Union Version (SUV)

Hakikisho la Msaada wa Mungu na Ombi la Uponyaji

1. Heri amkumbukaye mnyonge;BWANA atamwokoa siku ya taabu.

2. BWANA atamlinda na kumhifadhi hai,Naye atafanikiwa katika nchi;Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake.

3. BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani.Katika ugonjwa wake umemtandikia.

4. Nami nalisema, BWANA, unifadhili,Uniponye roho yangu maana nimekutenda dhambi.

5. Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya,Atakufa lini, jina lake likapotea?

6. Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo,Moyo wake hujikusanyia maovu,Naye atokapo nje huyanena.

7. Wote wanaonichukia wananinong’ona,Wananiwazia mabaya.

8. Neno la kisirani limemgandama,Na iwapo amelala hatasimama tena.

9. Msiri wangu tena niliyemtumaini,Aliyekula chakula changu,Ameniinulia kisigino chake.

10. Lakini Wewe, BWANA, unifadhili,Uniinue nipate kuwalipa.

11. Kwa neno hili nimejua ya kuwa wapendezwa nami,Kwa kuwa adui yangu hasimangi kwa kunishinda.

12. Nami katika ukamilifu wangu umenitegemeza,Umeniweka mbele za uso wako milele.

* * *

13. Na atukuzwe BWANA, Mungu wa Israeli,Tangu milele hata milele. Amina na Amina.